Netanyahu anataka kuingia kwenye vita vya kieneo na Iran. Je, ni kwa nini? Israel ilipoushambulia kwa bomu ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria wiki mbili zilizopita, na kumuua shahidi jenerali wa ngazi ya juu wa Iran, ilianzisha kwa makusudi mlolongo wa matukio yaliyopangwa kwa utaratibu maalumu kwa ajili ya kuisukuma Iran vitani. Iran ililipiza kisasi cha ulipuliwaji ubalozi wake tarehe 14 Aprili.